Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Bodi ya Pamba Tanzania

Leseni ya kununua pamba mbegu

Imewekwa: 26 February, 2026

Mdau wa pamba anayehitaji kuingia katika biashara ya kununua na kuchambua pamba mbegu anapaswa kuwa na vielelezo vifuatavyo ili aweze kupata leseni ya kununua pamba mbegu

  • Leseni ya mfanyabiashara
  • Udhibitisho wa uanachama wa chama cha wafanyabiashara wa pamba (TCA)
  • Kibali kutoka halmashauri ya wilaya husika
  • Udhibitisho wa kumiliki au kukodi kiwanda cha kuchambua pamba mbegu

Maombi yote yawasilishwe Bodi ya Pamba Tanzania kupitia mfumo wa mtandaoni kwa tovuti ya

https://ekilimo.kilimo.go.tz/